NA JANET KAVUNGA
CHANGAMWE, MOMBASA
JAMAA wa hapa alimtema demu wake kwa kumtaka aonje tunda siku ya kwanza ya date yao.
Alishangazwa na demu huyo kumtaka wakodishe chumba wakeshe licha ya kuwa hakuwa amemfahamu vyema.
“Alionekana kupandwa na mzuka lakini sikuingia boksi yake. Nilishuku mbio zake hizo za kutaka kunionjesha tunda na nikamtema mara moja,” jamaa alisema na kuungwa mkono na wenzake,
japo baadhi walimkejeli kwa kuogopa kutafuna tunda.