• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 3:09 PM
Sitaki kusikia habari zenu, demu aambia mapolo ‘stingy’

Sitaki kusikia habari zenu, demu aambia mapolo ‘stingy’

NA JANET KAVUNGA

MOMBASA MJINI

MWANADADA wa hapa, aliwakemea wanaume wawili waliokuwa wakimmezea mate akiwalaumu kwa kuwa mkono gamu.

Demu alikuwa akirushiwa mistari na wanaume hao kwa muda, lakini hakuna aliyempa miadi ya maana huku wakikutana katika bustani za umma.

Juzi, demu aliwapa mtihani kwa kutaka kila mmoja wakutane katika kilabu kimoja maarufu mjini hapa.

Katika miadi na jamaa wa kwanza, alimtaka ampeleke shopping lakini akaruka akisema alikuwa na mkutano wa dharura.

Katika miadi na jamaa wa pili, demu alijifanya mgonjwa na jamaa akamtaka aende hospitalini badala ya kujitolea kumpeleka.

Ni baada ya matukio hayo ambapo demu aliandikia kila mmoja ujumbe akimkemea na kumtaka amkome.

  • Tags

You can share this post!

Mwanamitindo Milka Mukami kuwakilisha Kenya kwa shindano la...

Viongozi 001 waahidi kushirikiana na EACC, ripoti ikitaja...

T L