Na LEAH MAKENA
SOUTH C, NAIROBI
WAREMBO katika kanisa la hapa walishangaza washiriki walipoangushana chini wakipigania gari la kiongozi wa vijana.
Duru zasema kuwa polo mwenye gari alipata kazi yenye mshahara mnono na kufanya warembo wengi kuanza kummezea mate.
Siku ya tukio, warembo hao walihudhuria ibada kama kawaida ila wakashangaza kung’ang’ania kiti cha mbele cha gari la polo punde tu ibada ilipokamilika.
Vuta nikuvute kati ya warembo hao ilianza waliporushiana cheche za matusi na kupigana kila mmoja akidai polo alikuwa chali wake.
Ilibidi akina mama waingilie kati kutenganisha wawili hao na kuwakaripia vikali.
“Mbona mnajiaibisha kwenye uwanja wa kanisa? Kama mnataka drama tokeni nje, tumechoka na vituko vyenu”.