NA TITUS OMINDE
MSHUKIWA wa ubakaji anayedaiwa kuwaibia na kuwabaka wanawake katika miji ya Eldoret, Kitale, Bungoma jana Jumatano alichiliwa kwa dhamana ya Sh500,000 baada ya kukana mashtaka.
Abdi Kele Duncan,26, ambaye amehusishwa na visa kadhaa vya kuwabaka wanawake na kuwaibia vitu vya thamani, alikana kumuibia mwathiriwa zaidi ya Sh19,000.
Alikana mashtaka na kuachiliwa kwa bondi ya Sh500,000 na mdhamini sawa. Mahakama ilipinga kuachiliwa kwa dhamana ya pesa taslimu.
Kesi hiyo itatajwa Aprili 14 ili isikilizwe mapema.