• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 12:38 PM
Anayedaiwa kubaka na kuiba apewa dhamana

Anayedaiwa kubaka na kuiba apewa dhamana

NA TITUS OMINDE

MSHUKIWA wa ubakaji anayedaiwa kuwaibia na kuwabaka wanawake katika miji ya Eldoret, Kitale, Bungoma jana Jumatano alichiliwa kwa dhamana ya Sh500,000 baada ya kukana mashtaka.

Abdi Kele Duncan,26, ambaye amehusishwa na visa kadhaa vya kuwabaka wanawake na kuwaibia vitu vya thamani, alikana kumuibia mwathiriwa zaidi ya Sh19,000.

Alikana mashtaka na kuachiliwa kwa bondi ya Sh500,000 na mdhamini sawa. Mahakama ilipinga kuachiliwa kwa dhamana ya pesa taslimu.

Kesi hiyo itatajwa Aprili 14 ili isikilizwe mapema.

You can share this post!

Wanjigi sasa apata makao mapya Safina

Azimio yavuna Mlimani Kiraitu akitangaza kumuunga Raila

T L