• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 12:25 PM
DONDOO: Mke amchemkia mumewe kwa ‘kumla’ kisura kwa macho

DONDOO: Mke amchemkia mumewe kwa ‘kumla’ kisura kwa macho

KILIFI MJINI

Na JANET KAVUNGA

MWANADADA aliyekuwa shopping na mumewe alilipuka kwa hasira kufuatia tabia ya jamaa huyo ya kukazia macho vipusa.

Demu alikerwa na jamaa alipokodolea macho makalio ya kipusa aliyekuwa mbele yao kwenye foleni wakisubiri kulipia bidhaa katika supermarket.

“Ikiwa unakula kwa macho tukiwa pamoja, itakuwaje ukiwa peke yako,” demu alifoka.

Na wakati huo huo huko Diani mjini Kwale, jamaa mmoja hakuamini alipopata habari kwamba demu aliyenuia kuoa alikuwa akifanya harusi siku tatu baada ya kukesha naye katika hoteli moja eneo hili.

Jamaa alikuwa kazini rafiki yake alipomtumia kadi ya harusi ya demu huyo na mwanamume mwingine.

Alishtuka hadi akashindwa kufanya kazi na kuomba ruhusa apate nafasi ya kuenda kuthibitisha akidhani rafiki huyo alikuwa akimfanyia mzaha.

Alipompigia demu simu, alithibitisha kwamba alikuwa akiolewa katika harusi na akamfahamisha kwamba alikuwa amemuaga rasmi walipokesha hotelini.

“ Nilitumia deti yetu hotelini kukuaga na siku tatu zijazo nitakuwa mali ya mwanamume mwingine.

Pokea shukrani zangu kwa muda ambao tumekuwa wapenzi. Nakutakia kila la heri unaposaka ubavu wako wa halali,” demu alimwambia polo bila kujutia kwamba alimchezea shere kwa miaka minne.

  • Tags

You can share this post!

Ababu ashambuliwa na wenzake UDA kwa “kutelekeza...

‘Mathe halisi wa Ngara’ atiwa mbaroni

T L