• Nairobi
  • Last Updated May 8th, 2024 6:50 AM
Habari ndio hiyo!

Habari ndio hiyo!

KATIKA miaka ya hivi karibuni, tasnia ya Showbiz imeanza kushuhudia maceleb wengi walio kwenye mahusiano ya jinsia moja, wakipata ujasiri na kujitokeza wazi wazi.

Licha ya matusi, masimango, kukashifiwa, kusutwa na chambo kibao wanazokutana nazo, baadhi yao wameamua kusimama kidete na kutetea desturi hii mpya inayotafsiriwa kuwa ya Kimagharibi zaidi. Hapa nchini, mahusiano ya jinsia moja hayatambuliwi hata kikatiba.

Pamoja na kuwa wanapata upingamizi mkubwa na unyanyapaa, pia wanapata sapoti kutoka kwa Mashirika tofauti ya kutetea haki za binadamu, mashabiki na hata wadau mbalimbali waliopo kwenye tasnia.Hawa ni baadhi tu ya maceleb walioweza kujitokeza waziwazi na kutangaza kuwa wapo kwenye mahusiano ya jinsia moja.

MAKENA NJERI: Kwa miaka mingi tu mwigizaji na produsa wa zamani wa BBC na NTV Chris Makena Njeri amekuwa akishukiwa kuwa ni msagaji.

Mwezi uliopita, alithibitisha tetesi hizo alipotokea katika kipindi cha TedX Parklands. Kwenye kipindi hicho, Makena alisema imemchukua miaka mingi kuja kujikubali kuwa yeye ni msagaji.Aidha mwigizaji huyo wa zamani katika kipindi cha Tahidi High, alisema alikuwa akiona haya kila alipokuwa akijitambulisha.

‘Nakumbuka kwa mara ya kwanza katika maisha yangu baada ya miaka mingi nikijitizama kwenye kioo, niliishia kujisemea moyoni mimi ni msagaji, mimi ni mtu tofauti na huo ndio ukweli wangu,’ Njeri alisema kwenye kipindi hicho.

Vile vile alizungumzia kisanga cha 2019 ambapo alitrendi baada ya aliyekuwa mpenzi wake kufanya uharibifu mkubwa kwenye gari lake aina ya Mercedes Benz baada ya kumshuku kuwa alikuwa akimhanyia.

NOTI FLOW: Rapa huyu hajawahi kuyaficha mahusiano yake. Amekuwa kwenye mahusiano na wanawake pamoja na wanaume.

Lakini baada ya Makena kujitokeza, Noti alipata ujasiri wa kujitokeza na kusema kwa sasa yupo kwenye mahusiano na demu mwenzake baada ya mahusiano yake na Colonel Moustapha kuingia mdudu.

Alisema kila kitu alichokuwa akitaka kutoka kwa mahusiano yake yaliyopita na mwanaume alikosa lakini akayapata kwa mpenzi wake wa sasa King Alami. Mapenzi baina yao yamewazidia na tayari wanaishi pamoja.

KAREN KAZ: Mwanamuziki Karen yupo kwenye mahusiano na sio tu demu mmoja lakini wawili. Mwezi uliopita, Karen aliposti video akilishana udenda na mmoja wa wapenzi wake kwa jina Majic Dyke.

Ilikuwa ni sehemu ya kusherehekea uhusiano wao wa miezi sita toka wawe wapenzi. Lakini pia Majic mwenyewe alithibitisha kuwa yupo kwenye uhusiano mwingine na mwanamke mzungu Dame Yankee.Watatu hawa wanafahamiana vizuri tu na mara kwa mara wao hukutana wote kufurahia mapenzi yao.

BINYAVANGA WAINAINA: Marehemu Wainaina alikuwa ni mwanahabari na mwandishi wa vitabu mashuhuri. Lakini pia alikuwa ni mwanaharakati na mtetezi mkubwa wa watu waliopo kwenye mahusiano ya jinsia moja.

Wainaina aliyeshinda tuzo la Caine Prize 2002 kutokana na uandishi wake, aliweka wazi mahusiano akijitangaza kuwa shoga. Kabla ya kufariki dunia 2019, alikuwa kwenye harakati za kufunga ndoa na mchumba wake wa miaka mingi a wa Nigeria.Alijitokeza na kutangaza kuwa ni shoga 2014 kwenye stori aliyoandika na kuipa kichwa Mama mimi ni shoga.

Ilikuwa ni barua ya wazi kwa mamake aliyekuwa mgonjwa wakati huo. Baadaye alitupia twiti akikariri kuwa ni shoga na mahusiano yake yalikuwa ya furaha tu.Gazeti la Time Magazine liliwahi kumworodhesha kuwa miongoni mwa watu 100 wenye ushawishi mkub

  • Tags

You can share this post!

Ondoa chunusi usoni kwa kutumia maji ya mshubiri(Aloe vera).

Teuzi zote zifanywe kwa kuzingatia katiba bila ubaguzi