• Nairobi
  • Last Updated May 7th, 2024 9:48 PM
Hawara achomea picha vidume wa Man U akidai wote ni mafisi wa kutupwa

Hawara achomea picha vidume wa Man U akidai wote ni mafisi wa kutupwa

Na CHRIS ADUNGO

MWANAMITINDO maarufu mraibu wa TikTok ambaye kwa sasa ni kahaba, Sky Bri, ameduwaza wengi kwa kudai kuwa idadi kubwa ya wanasoka wa Manchester United wanamvizia kimapenzi mitandaoni.

Mrembo huyo pia hunadi picha za uchi na filamu za ngono kwa malipo kupitia jukwaa la ‘OnlyFans’.

Katika mahojiano na gazeti la The Sun wiki hii, alikiri kutoza wateja hadi Sh5,400 kwa picha moja huku video moja ikigharimu pesa zisizopungua Sh18,000 kutegemea “ambacho mteja anataka kuona na kufurahia katika mwili wake”.

“Yaonekana kazi ninayoifanya inavutia sana wachezaji wa pale ugani Old Trafford. Wengi wao wamekuwa wakinifikia kikashani (DM), kila mmoja akiomba nafasi ya kudokoa tunda langu hili,” akasema.

Ungamo la Sky lilifurahisha idadi kubwa ya mashabiki mitandaoni na mmoja wao akachochewa kusema: “Simlaumu yeyote kati ya wanasoka hao wanaomvizia. Hata mimi ni ‘fisi hatari’. Naomba nitangulie kisimani kabla wakufikie!”

Aidha, alifichua kwamba jeshi kubwa la wafuasi na ‘mafisi’ wanaomfukuzia mitandaoni ni masogora maarufu wa Man-United ambao sasa humtumia jumbe za moja kwa moja kikashani (DM) wakitaka fursa ya kutoka naye kimapenzi.

“Yaonekana kazi ninayoifanya inavutia sana wachezaji wa pale ugani Old Trafford. Wengi wao wamekuwa wakinifikia kikashani (DM), kila mmoja akiomba nafasi ya kudokoa tunda langu hili,” akasema.

Ungamo la Sky lilifurahisha idadi kubwa ya mashabiki mitandaoni na mmoja wao akachochewa kusema: “Simlaumu yeyote kati ya wanasoka hao wanaomvizia. Hata mimi ni ‘fisi hatari’. Naomba nitangulie kisimani kabla wakufikie!”

Mwingine alisema: “Man-United ni klabu ya mafisi wakubwa. Sijaelewa kiini cha hilo. Cha kufurahisha ni kwamba yawezekana anayemtamani Sky kutoka kule Trafford ni mwanasoka yeyote! Naomba utaje majina.”

Shabiki wa tatu aliongeza: “Sisi ni wa pekee kabisa. Nani kama sisi! Tuishi kwa muda mrefu Man-United ili tutambe ugani na pia chumbani!”

Kuhusu uhusiano wake na Paul na kiini cha kusambaratika kwa penzi lao, Sky alisema: “Alishindwa kazi usiku wa kwanza kabisa nilipomfungulia mzinga wa asali alioishi kuomba kwa muda mrefu hata kabla tufahamiane vizuri. Alikera zaidi alipotaka nipigwe naye picha akinibusu, kisha nipakie mitandaoni ili ijulikane nilimwonjesha.”

  • Tags

You can share this post!

Kijana, 20, aondolewa kesi ya ubakaji baada ya kudhihirisha...

Serikali imepunguza kwa asimilia 50 bajeti ya usafiri...

T L