• Nairobi
  • Last Updated May 6th, 2024 3:46 PM
Mmoja aokolewa Shakahola

Mmoja aokolewa Shakahola

Na ALEX KALAMA

MTU mmoja ameokolewa Jumapili katika oparesheni ya kutafuta manusura waliosalia katika msitu wa Shakahola, Kaunti ya Kilifi.

Idadi hiyo inafikisha jumla ya waliookolewa kuwa watu 46.

Kupitia taarifa iliyotolewa na idara ya usalama, idadi ya waliokamatwa kwa kuhusishwa na matukio ya maafa eneo hilo pia imeongezeka hadi watu 23.

Hata hivyo, taarifa hiyo imebainisha kuwa idadi ya miili ya watu iliyopatikana katika eneo hilo imefikia 110 baada ya mwili mmoja zaidi kupatikana hapo jana.

Haya yanajiri huku shughuli ya upasuaji wa miili iliyofukuliwa eneo hilo ikitarajiwa kuanza juma hili.

Paul Mackenzie, mhubiri tata anahusishwa na maafa yaliyoandikishwa.

Kwa sasa angali anazuiliwa na polisi uchunguzi ukiendelea.

Vyombo vya habari vilipigwa marufuku dhidi ya kufuatilia oparesheni hiyo mbashara.

 

  • Tags

You can share this post!

Kundi la Azimio Magharibi mwa Kenya lajitenga na maandamano...

Raila akaa ngumu kuhusu maandamano 

T L