• Nairobi
  • Last Updated May 7th, 2024 9:48 PM
Mwanachama wa Mungiki atisha kuua landilodi

Mwanachama wa Mungiki atisha kuua landilodi

Na RICHARD MUNGUTI

MWANACHAMA wa chama kilichopigwa marufuku cha Mungiki ameshtakiwa kutisha kumuua landilodi wake katika mtaa wa Dagoreti , Nairobi.

Anthony Muchiri Nduta anakabiliwa na shtaka la kutisha kumuua Charles Samuel Karugu mnamo Agosti 15 2021.Alipofikishwa mbele ya hakimu mkazi Sharon Maroro, mshtakiwa alidaiwa alimtisha Karugu akisema,“utanjua mimi ni Mungiki, nitakuua leo.”

Karugu alikuwa amemwitisha Nduta ada ya nyumba.Mshtakiwa alilalamika hana pesa za kulipia nyumba kwa vile hakuwa kazini.Mshtakiwa alidaiwa alikuwa amemtupia mlalamishi Sh1,000 kisha akaziokota baada ya kumsukuma.Baada ya vurugu ya muda kidogo, mshtakiwa na mlalamishi waliachana na kila mmoja kwenda zake

Hatimaye, Nduta anadaiwa alimfuata Karugu kilabu alipokuwa ameenda kutazama kandanda.Alimtokea mlalamishi akiwa amebeba upanga na kutisha kumuua.Karugu aliondoka mahala hapo baada ya mshtakiwa kuzua vurugu tena.Nduta alienda kwenye duka la mlalamishi huku akitisha aidha amuue mkewe mlalamishi ama Karugu.

Wateja walichomoka dukani kwa mwendo wa kasi mithili ya farasi.Mshtakiwa alikutwa kwenye duka la mlalamishi akiwa amejihami kwa upanga.Aliachiliwa kwa dhamana ya Sh30,000 pesa tasilimu.

  • Tags

You can share this post!

MKU yapokezwa cheti maalum kwa kutambulika kama kituo rasmi...

Dereva atozwa faini ya Sh70000 kwa kumuua mwanafunzi