• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 6:07 PM
Siku Kibaki alikosa sahani katika hafla ya Moi

Siku Kibaki alikosa sahani katika hafla ya Moi

Na FRANCIS MUREITHI

HAYATI Mzee Mwai Kibaki alilazimika kula chakula kwenye sufuria baada ya kukosa sahani alipochelewa kufika katika hafla ya Rais Daniel Moi.

Kulingana na katibu wa muda mrefu wa Mzee Moi, Lee Njiru, Kibaki alikula moja kwa moja kutoka kwenye sufuria katika hafla hiyo iliyokuwa ikifanyika mjini Wote, Kaunti ya Machakos.

“Kibaki alipata mimi na mlinzi wa Rais Moi Wilson Boinett tunakula. Bila kupoteza wakati, Kibaki alichukua sufuria na kuanza kula chakula kwani hakukuwa na sahani,” akasema Bw Njiru.

Alisema alikwepa meza alikokuwa Moi kwa sababu hakutaka ijulikane alichelewa kufika.

“Vilevile, ninakumbuka alipokuwa akifanya kampeni Embu mnamo 2002, nilikutana naye hotelini. Nilijaribu kumkwepa kwa sababu sikutaka anione kwa kuwa alikuwa katika upinzani. Aliponiona, alinimiminia sifa tele huku akisema ‘mimi huwa sielewi mambo ya Moi hadi nisome magazetini. Lakini Njiru anamuelewa. Watu wa Embu mmebarikiwa kuwa na mtoto (Njiru) anayemwelewa Moi’,” akasema.

Mzee Njiru alimtaja Kibaki kama mcheshi ambaye hakupenda kufuata upepo wa wanasiasa wengine.

  • Tags

You can share this post!

Presha kwa Ruto na Raila kuhusu wagombea wenza

Ujenzi wa kituo cha kisasa kutoa mafunzo na huduma za...

T L