• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 5:29 PM
Gachagua awataka Wakenya kumuombea Kenyatta kukubali Ruto ndiye Rais     

Gachagua awataka Wakenya kumuombea Kenyatta kukubali Ruto ndiye Rais    

 

NA MWANGI MUIRURI

NAIBU wa Rais Rigathi Gachagua amewataka Wakenya wamuombee Rais mstaafu Uhuru Kenyatta “awe na roho kukubali Rais William Ruto ndiye kinara wa Kenya”.

Alisema kwamba “ninatumana kazi kwa Wakenya wote walio na nyota ya maombi watusaidie kumwombea Rais huyu wetu mstaafu ili akome tabia zingine ambazo tumekuwa tukishuhudia kutoka kwake”.

Ingawa Bw Kenyatta wiki iliyopita alisema kwamba “Ruto ni Prezzo wangu na akiniita nikutane na nijadiliane naye nitakwenda, Bw Gachagua alisema “bado hajakubali uamuzi wa Mungu kwamba Ruto ndiye Rais kwa wakati huu”.

Bw Gachagua akiongea katika hafla ya maombi ya pamoja katika Ikulu ndogo ya Sagana, Nyeri mnamo Jumapili, Agosti 6, 2023 alisema kwamba “tumuombee akome tabia mbovu kama za kufadhili maandamano, uharibifu wa nchi na masuala mengine yasiyo ya ustaarabu”.

Hata hivyo, Bw Kenyatta amekuwa akisisitiza kwamba yeye huunga mkono mrengo wa upinzani lakini huwa hashiriki maandamano wala kujiingiza katika visa visivyoambatana na sheria.

Bw Gachagua alisema kwamba yalikuwa mapenzi ya Mungu Dkt Ruto ashinde kura ya Agosti 9, 2022.

“Viziki tulivyokuwa tumewekewa havingerukwa kwa uwezo wetu. Huo ulikuwa mkono wa Mungu. Kwanza Mimi sikuwa katika hali nzuri.

“Walikuwa wakinikamata Ijumaa na kuniachilia Jumatatu. Mlitufanyia muujiza, hasa mimi binafsi kwa kutupa kura zenu. Mlitunusuru njama hatari,” akasema.

Kama shukrani, Bw Gachagua aliwatuza baadhi ya wenyeji mlo wa nyama na wali katika Ikulu ya Sagana huku akiwaambia hata ile nyingine ya kuwatuza uji katika boma lake binafsi ipo njiani yaja.

 

[email protected]

 

  • Tags

You can share this post!

Akothee aibua hisia mseto mtandaoni baada ya Askofu Mkuu...

Wito wa viongozi wa kidini Kisii Rais Ruto na Odinga...

T L