• Nairobi
  • Last Updated May 6th, 2024 8:55 PM
Baha achukua mapumziko mafupi mitandaoni

Baha achukua mapumziko mafupi mitandaoni

NA MERCY KOSKEI

MUIGIZAJI wa zamani wa Kipindi cha Machachari, Tyler Mbaya maarufu kama Baha ametangaza kuwa anachukua mapumziko ya muda kwenye mitandao ya kijamii ili kupata matibabu.

Kipindi hicho hupeperushwa na runinga ya Citizen.

Kupitia akaunti yake ya Instagram, Baha amesema kuwa anaanza ukurasa mpya wa maisha yake.

“Wagwan Tyler. Doc anahisi kama nahitaji mapumziko madogo mitandaoni kama njia ya kuondoa ‘sumu mwilini’ ninapoanza safari yangu ya kupona. Ninakubali…Ninahitaji kutanguliza afya yangu ya akili. Kwa hivyo nitachukua hatua mbili- mapumziko ya wiki mbili ili kuniruhusu kuwa na mwanzo mzuri. Nitarudi hivi karibuni,” alinukuu.

Tyler mnamo Ijumaa, Juni 9, 2023 kwenye mkutano na waandishi wa habari alikiri kuwa na tatizo la kucheza kamari, huku akifunguka kuwa anakabiliwa na aibu kwa tabia yake na sasa ametafuta usaidizi wa kurekebisha.

Alisema kuwa kikao chake cha kwanza cha matibabu kilimsaidia, akiwaonya wenzake dhidi ya tabia hiyo mbaya – kucheza kamari.

Tyler alianikwa mapema wiki jana na Mkenya mmoja nchini Amerika, aliyedai kuwa alimlaghai Sh20, 000.

Muuguzi Judy anayeishi Amerika alibaini kuwa mwigizaji huyo alimkopa pesa za kulipa bili, baada ya kudai kuwa alikuwa hajalipa kodi kwa muda.

Hata hivyo, madai hayo yalimkera mke wa Baha, Georgina ambaye alifichua kuwa hulipa bili na kwamba Baha ana tatizo la kucheza kamari.

Ufichuzi huo uliwaacha Wakenya vinywa wazi, huku wakishauri Judy kutafuta njia nyingine ya kurejesha pesa zake.

Baadaye video ya muziki iliyowashirikisha Baha na Georgina iliachiliwa.

Wimbo wa Jovial na Lexsil uliibua maswali huku wengi wakisema kuwa ilikuwa mbinu kusaka ufuasi mkubwa mitandaoni.

  • Tags

You can share this post!

Joseph Yobo aamini Kenya ina wanasoka wenye uwezo wa...

Kitendawili cha nyanya kupatikana ‘amejinyonga’ akiwa...

T L