• Nairobi
  • Last Updated May 8th, 2024 8:50 AM
Nina wawili ila kwa sasa mwenzenu niko singo, adai Samidoh

Nina wawili ila kwa sasa mwenzenu niko singo, adai Samidoh

NA FRIDAH OKACHI

WATUMIAJI wa mitandao ya kijamii wanaofuatilia maisha ya wasanii wamebaki vinywa wazi baada ya mwanamuziki Samuel Muchoki almaarufu Samidoh kudai hana mpenzi licha ya wao kufahamu ana wanawake wawili kwenye maisha yake ya mahusiano.

Edday Nderitu anafahamika kuwa mke wake rasmi lakini alimuacha Samidoh na kuenda nchini Marekani anakofanya kazi na kuhakikisha wanawe wanapata elimu katika nchi hiyo.

Kabla ya mkewe kuondoka, mwanamuziki huyo alikuwa ameazisha mahusiano na Seneta Maalum Karen Nyamu ambaye walifanikiwa kupata watoto wawili.

Katika video moja aliyokuwa akizungumza na mashabiki wake, mwanamuziki huyo alisikika akisema kwa sasa hivi hana mtu.

“Licha ya kuwa mwanamume aliye na wake wawili, sasa hivi niko singo,” alisema Samidoh akitabasamu.

Kauli hiyo ilifanya wengi kuamini wawili hao – Samido na Karen – hawako pamoja.

Samidoh, aliongeza kuwa ameweka kizuizi bila ya kutaja ni nani amewekewa.

“Yuko kwa block list,” alibainisha Samidoh.

Baadhi ya watumiaji mitandao wakaanza kutoa maoni yao.

Eve Naomi alishangazwa na kipindi kifupi cha mahusiano yao, akisema wakati wa mahusiano ya aina hiyo huwa miaka miwili.

“Umekuwa muda mfupi sana… huwa tunawapa miaka miwili na baadaye tunajiuliza iwapo kumekuwa na umuhimu wowote?” akasema Eve Naomi.

The_Nthenya alichangia kwa kuonya kuwa mwanamuziki huyo hapendi.

“Jamaa hapendi mtu yeyote, ni yeye tu. Kwa hivyo Bi Nyamu asione kuwa ni mzuri kumliko Edday,” akachangia The_Nthenya.

Veronika Tibwa akasema kuwa kwa muda mrefu, mwanamuziki huyo hajakuwa akitrendi kwenye majukwa ya mitandao ya kijamii na hivyo basi kutumia kauli hizo ni kutaka kuwa maarufu tena.

“Hajakuwa aki-trend, sasa anatafuta mbinu,” alichangia Veronica Tibwa.

Mnamo Novemba 2023, Samidoh na Bi Nyamu kila mmoja aliacha kumfuata mwezake kwenye ukurasa wa Instagram. Hali hiyo ilifanya wengi kujiuliza iwapo wawili hao wameachana au wangali kitu kimoja.

Mapema Jumatatu wiki jana, mashabiki walibainisha mwanamuziki huyo amerejea kuwa mfuasi wa mkewe Bi Nderitu kwenye ukurasa wa Instagram.

  • Tags

You can share this post!

Hofu Pokot Magharibi takwimu za matineja wanaopachikwa...

Kang’ata aandika barua akilia kuhusu kuharibika kwa...

T L