• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 2:03 PM
Caroline ajivunia kuwa mwingizaji

Caroline ajivunia kuwa mwingizaji

Na JOHN KIMWERE

NI miaka minne tangia aanze kujituma kwenye masuala ya uigizaji ambapo anasema amepania kutinga hadhi ya juu katika tasnia ya maigizo.

Caroline Wanjiru Muthoni maarufu CM ni dada anayejivunia kuvalia kofia kadhaa licha ya umri wake mdogo. Kando na uigizaji binti huyu anajihusisha na biashara tofauti ikiwamo kuuza magari, biashara ya nyumba za kifahari pia anamiliki kampuni ya CM Productions.

Ni brandi aliyoianzisha mwaka 2018 inayojihusisha na masuala ya kutayarisha na kurekodi muziki wa audio na video pia kuandaa hafla za harusi kati ya zingine. ”Hakika ilikuwa furaha tele kwangu mwaka 2018 niliposhiriki kipindi cha Auntie boss na kubahatika kupeperushwa kupitia runinga ya NTV,” amesema na kuongeza kuwa hatua hiyo ilimtia motisha zaidi kuzamia zaidi katika masuala ya maigizo.

Binti huyu aliyezaliwa mwaka 1995 anasema alivutiwa na uigizaji baada ya kutazama filamu iitwayo Sunset Boulevard. Ni filamu kuhusu malkia wa filamu aliyekataa kukubali kuwa nyota yake katika uigizaji imefifia. Tangia nikiwa mtoto nilitamani kuhitimu kuwa mwana habari lakini baada ya ndoto hiyo kuyeyuka ninalenga kuibuka mwigizaji mashuhuri duniani.

”Katika mpango mzima barani Afrika nimepania kufuata nyayo za muigizaji songora Viola Davis mzawa wa Marekani aliyeshiriki filamu kwa jina ‘Fences,’ akasema. Anadokeza kuwa kupitia brandi yake analenga kuzalisha filamu zitakazobadilisha maisha ya wengi hapa duniani kwa jumla bila kuweka katika kaburi la sahau kutoa ajira kwa waigizaji chipukizi wavulana na wasichana.

Mwigizaji Caroline Wanjiku Muthoni… Picha/JOHN KIMWERE

Binti huyu anajivunia kushiriki filamu kadhaa ambazo zimepata mpenyo kupeperushwa kupitia runinga tofauti nchini. Baadhi yazo zikiwa: Auntie Boss (NTV), Varshita (Maisha Magic East), Tuikaranie -Tuishi pamoja (Kameme TV) na Ofisi Show (Baze TV).

THANDO THABETE

”Ndio nimeanza kupiga ngoma katika uigizaji lakini ninafahamu ni ajira kama nyingine maana tayari ninajivunia matunda ya taaluma yangu,” akasema.

Barani Afrika angependa kufanya kazi na waigizaji kama: Thando Thabete mzawa wa Afrika Kusini aliyeshiriki filamu kama ‘Housekeepers’ na ‘How to ruin Christmas’ kati ya zinginezo. Duniani yupo mzawa wa hapa nchini, Lupita Nyong’o anayezidi kutesa katika tasnia ya filamu za Hollywood aliyeshiriki ‘Black Panther,’ na ‘Queen of Katwe.’ Hapa nchini angependa kufanya kazi nao Brenda Wairimu ‘Disconnect,’ na ‘Monica,’ pia Kate Actress ‘Nafsi’ na ‘Sue and Johnny.’

MIAKA MITANO

Anasema ndani ya miaka mitano ijayo chini ya brandi yake analenga kuzalisha filamu mbili na nyimbo kadhaa za video. Anatoa wito kwa serikali na kusema inastahili kuweka mikakati kabambe iili kuwapa wana maigizo moyo. ”Pia sina shaka kutaja kuwa inapaswa kuweka mandhari ya kuvutia maprodusa wengi kushuti video hapa nchini,” akasema.

Anashauri wenzake wasife moyo na wawe wakamavu pia wafahamu wanachotaka katika sekta ya burudani. Kadhalika anawahimiza wawe wabunifu kama wenzao katika mataifa yanayoendelea.

Mwigizaji Caroline Wanjiku Muthoni…Picha/JOHN KIMWERE
  • Tags

You can share this post!

Amazon Ladies imani ipo siku itawika katika handiboli

Shari Afrika awaza kubeba tuzo ya Grammys

T L