NA MARGARET MAINA
Muda wa kuandaa: Dakika 30
Muda wa mapishi: Dakika 50
Walaji: 2
Vinavyohitajika
Maelekezo
Loweka mchele: Suuza mchele hadi maji yaonekane safi, kama dakika nne. Mimina maji baridi ya kutosha ndani ya bakuli ili mchele uzame kabisa. Ongeza mchele na loweka mchele kwa angalau dakika 10.
Karanga viungo kwenye sufuria juu ya moto wa kati. Utaanza kwa kumimina mafuta halafu ukoroge karafuu, iliki, mdalasini, na pilipili nyeusi.
Mara tu viungo vinapoanza kuiva, ongeza vitunguu. Kaanga vitunguu kwa muda wa dakika nane au hadi viwe na rangi ya dhahabu. Kisha ongeza chumvi. Koroga mara kwa mara ili kuzuia kuungua. Punguza moto hadi kiwango cha chini, kisha kaanga vitunguu saumu, tangawizi, pilipili na korosho (ikiwa unatumia) hadi hivi vyote viwe na harufu nzuri.
Ongeza nyanya, garam masala, na binzari. Pika kwa muda wa dakika tano hadi kioevu cha nyanya kipungue kidogo na kuanza kushikamana na sufuria.
Ongeza maji, mchele na kijiko 1 cha chumvi.
Acha mchanganyiko uchemke hadi viputo vitengenezeke juu – ni kama dakika tano.
Koroga wali mara moja (unaweza kuona sehemu ya chini ya mchele imeshikamana kidogo na sufuria; koroga kwa uangalifu ili kulegeza nafaka yoyote iliyokwama).
Ikiwa unatumia jiko la gesi, punguza moto kuwa wa chini. Funika sufuria na upike kwa dakika 20. Zima moto, kisha acha mchele utulie kwa dakika 10 ukiwa umefunikwa.
Ondoa kifuniko na upindue mchele kwa uma.
Nyunyizia majani ya giligilani kwa juu na pakua wali ukishaiva.