NA MARGARET MAINA
Muda wa kuandaa: Dakika 15
Muda wa mapishi: Dakika 20
Walaji: 2
Vinavyohitajika
Maelekezo
Kwenye kikaangio chako, mimina mafuta na chumvi na ongeza kwenye vitunguu maji vyekundu, mashina ya giligilani, tangawizi, vitunguu saumu, pilipili na maji ya limau. Pika hadi viwe laini na vyenye harufu nzuri.
Unaweza kuchagua kutotumia pilipili, au kuongeza zaidi au hata kidogo ikiwa unapenda. Ni kiungo cha hiari.
Subiri kwa muda kiasi hadi viive na viungo vyote vichanganyike pamoja. Katika hatua hii, mchuzi utakuwa mwekundu. Usiharakishe hatua hii kwani nyanya zinapaswa kuiva vizuri na viungo vinapaswa kuchanganyika vizuri.
Miminia krimu ya nazi na upike hadi mchuzi uwe mzito.
Ongeza majani ya giligilani kiasi na uyachanganye ndani. Chota mchuzi kiasi kwenye bakuli kisha ongeza samaki, na umwagilie sehemu ya mchuzi uliochota juu ya samaki. Acha samaki iive juu ya moto wa chini kwa dakika nyingine 10 hadi 15.
Hatua hii ni muhimu sana kwani inaruhusu ladha kujipenyeza ndani ya nyama na pia kuifanya iwe laini.
Mara tu ikiwa laini, pamba na majani mengine zaidi ya giligilani pamoja na limau iliyokatwa. Pakua na ufurahie.