NA MAGDALENE WANJA
MARUFUKU ya usafiri na kwenda kazini yaliadhiri watu wengi kisaikolojia wakati wa kanga la Covid-19.
Baadhi ya wafanyakazi walijipata katika hali ngumu zaidi haswa baada ya kuwapoteza wapendwa wao na mali.
Kulingana mwanasaikolojia Bi Faith Gichanga, mabadiliko hayo ambayo yalirekodi hali tofauti ya mazingira yalichangia pia katika msongo wa mawazo wa watu wengi.
Waajiri ambao walijitolea katika kuwatafutia wafanyakazi wao huduma za ushauru wa kisaikolojia waliweza kuokoa muda wa kuweza kurejesha hali zao za hapo awali.
“Idadi ya watu waliotaka huduma hizi iliongezeka sana wakati wa janga hilo na hata baada yake,” anasema Bi Gichanga.
Bi Gichanga anaongeza kuwa ni muhimu kwa mashirika na kampuni kuwarahisishia wafanyakazi wao mzigo wa kutafuta huduma hizi.
Huduma hizi hutozwa kati ya Sh3,000 na Sh20,000. Ada hizi hutegemea kama ni watu binafsi au makundi ya watu wengi.
Bi Gichanga anaongoza kuwa ingawa huduma za ushauri wa kisaikolojia ni muhimu kwa afya ya binafamu haswa kazini, bado hazijachukuliwa kwa uzito unaostahili.