• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 7:05 PM
Bayern Munich wakabwa koo na Eintracht Frankfurt na kuendeleza rekodi duni katika soka ya Bundesliga

Bayern Munich wakabwa koo na Eintracht Frankfurt na kuendeleza rekodi duni katika soka ya Bundesliga

Na MASHIRIKA

BAYERN Munich waliendelea kusuasua baada ya Eintracht Frankfurt kuwalazimishia sare ya 1-1 katika Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga) ugani Allianz Arena.

Sare hiyo ilikuwa ya tatu mfululizo na ya matokeo sawa kwa Bayern kusajili ligini. Baada ya kufungua mwaka huu kwa sare ya 4-4 dhidi ya RB Salzburg ya Austria kirafiki, miamba hao waliambulia sare ya 1-1 dhidi ya RB Leipzig katika Bundesliga kabla ya kusajili matokeo sawa na hayo dhidi ya Cologne.

Ni mara ya kwanza tangu 2007 kwa Bayern kutoshinda mechi nne mfululizo za ufunguzi wa mwaka mpya.

Hata hivyo, bado wanadhibiti kilele cha jedwali la Bundesliga kwa alama 37, moja zaidi kuliko nambari mbili Union waliopepeta Hertha 2-0 katika gozi kali la jiji la Berlin, Jumamosi. Frankfurt, ambao pia wamesakata mechi 18, wana pointi 32.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Barcelona wakomoa Girona na kukaa vizuri kileleni mwa...

Jinsi Manchester City walivyodengua Arsenal katika kipute...

T L