Na MASHIRIKA
CHELSEA wamemsajili beki wa kulia raia wa Ufaransa, Malo Gusto, 19, kutoka Olympique Lyon kwa kima cha Sh4.8 bilioni.
Gusto ametia saini mkataba wa mrefu utakaomdumisha ugani Stamford Bridge hadi mwaka wa 2030. Hata hivyo, atakamilisha kampeni za msimu huu wa 2022-23 akivalia jezi za Lyon watakaolipwa nyongeza ya Sh678 milioni.
Gusto alipokea malezi ya soka katika akademia ya Lyon kabla ya kuwajibishwa katika kikosi cha kwanza cha miamba hao kwa mara ya kwanza mnamo Januari 2021.
Kufikia sasa, Gusto amechezea Lyon wanaokamata nafasi ya tisa kwenye Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) mechi 15 msimu huu.
Mbali na Gusto, Chelsea wamejinasia pia huduma za wanasoka Noni Madueke, Mykhailo Mudryk, David Datro Fofana, Andrey Santos na Benoit Badiashile pamoja na Joao Felix aliyetokea Atletico Madrid kwa mkopo.
Gharama ya kujinyakulia maarifa ya wanasoka hao wote tayari imefikia kima cha Sh24.6 bilioni.
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO