• Nairobi
  • Last Updated May 8th, 2024 7:50 AM
Corona yavuruga mipango ya vikosi siku chache kabla ya kipute cha EPL kuanza

Corona yavuruga mipango ya vikosi siku chache kabla ya kipute cha EPL kuanza

Na MASHIRIKA

VINARA wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) wamethibitisha kwamba wanasoka tisa na baadhi ya maafisa wa klabu 20 zinazoshiriki kipute hicho wameambukizwa virusi vya corona chini ya kipindi cha wiki moja iliyopita.

Hali hiyo inatokea siku chache kabla ya kipenga cha kuashiria mwanzo wa msimu mpya wa 2021-22 kupulizwa rasmi mwishoni mwa wiki hii.

EPL ilifanya raundi mbili za vipimo 3,118 kati ya Agosti 2 na Agosti 8 ambapo visa tisa vya maambukizi ya corona vilipatikana.

Limbukeni Brentford waliopandishwa ngazi kushiriki EPL msimu uliopita wa 2020-21, wameratibiwa kufungua rasmi kampeni za muhula huu kwa gozi litakalowakutanisha Ijumaa ya Agosti 13 uwanjani Brentford Community.

Wasimamizi wa EPL wamesisitiza kwamba wataendelea kufanyia vikosi vyao vipimo vya corona mara mbili kwa wiki.

Kufikia sasa, maandalizi ya baadhi ya klabu za EPL kwa ajili ya msimu mpya wa 2021-22 tayari yamevurugwa na corona.

Arsenal walilazimika kufutilia mbali ziara yao ya kwenda kujinolea nchini Amerika huku Aston Villa, Manchester United na Chelsea wakisitisha pia michuano yao ya kirafiki.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Wanatenisi wa Kenya waanza mazoezi ya uwanjani baada ya...

Ruto akita kambi Nakuru kupigia debe mfumo wa kumuinua...