• Nairobi
  • Last Updated May 7th, 2024 9:48 PM
Italia na Argentina kuvaana kwenye mechi ya kuwania taji la Intercontinental Cup

Italia na Argentina kuvaana kwenye mechi ya kuwania taji la Intercontinental Cup

Na MASHIRIKA

MABINGWA wa Euro 2020 watakutana na washindi wa Copa America 2020, Argentina, kwenye mchuano wa Intercontinental Cup mnamo Juni 2022.

Hayo ni kwa mujibu wa Shirikisho la Soka la bara Ulaya (Uefa) ambalo limesisitiza kwamba mpango huo ni zao la maafikiano kuhusu kuandaliwa kwa makala ya tatu ya kivumbi hicho.

Japo vinara wa Uefa hawajafichua mahali na tarehe kamili ya kuandaliwa kwa gozi hilo, jiji la Naples nchini Italia tayari limependekezwa kuwa mwenyeji wa gozi hilo linalokutanisha wafalme wa soka ya bara Ulaya (Uefa) na wapambe wa kabumbu kutoka Amerika Kusini (Conmebol).

Mabingwa wa soka kutoka mabara hayo mawili wamekuwa wakikutana kila mwaka kuanzia 1960 kabla ya kivumbi hicho kuwa sehemu ya mashindano ya Fifa Club World Cup mnamo 2005.

  • Tags

You can share this post!

Alexander-Arnold na Maguire kutochezea Uingereza dhidi ya...

Club Bruges yaendeleza masaibu ya RB Leipzig kwenye UEFA