• Nairobi
  • Last Updated May 10th, 2024 6:24 PM
Kilifi Ladies yaanza Ligi ya Kanda kwa kishindo

Kilifi Ladies yaanza Ligi ya Kanda kwa kishindo

NA ABDULRAHMAN SHERIFF 

Ladies FC walianza mechi ya kwanza kabisa ya Ligi ya Kanda ya Pwani kwa matao ya juu walipokomoa mabingwa wa Kaunti ya Taita Taveta, Gicheha Queens FC, 2-0 katika uwanja wa Ziwani, Kaunti Ndogo ya Taveta, Jumamosi.

Kilifi ilifanikiwa kutia kibindoni alama zote tatu kupitia kwa mabao yaliyotingwa nyavuni na Annah Mwambire na Mary Mwambela.

Kocha Anthony Kadenge amesema wakiendelea na mchezo walionyesha, ana matumaini watashinda taji hilo.

Nayo Coast Starlets FC ya Kilifi ilipata pointi tatu baada ya wapinzani wao Chaani Ladies FC kukosa wachezaji wa kutosha ugani Changamwe.

Tunaomba radhi kwa timu za Coast Starlets FC  na Chaani Ladies FC kwa kuandika katika gazeti letu la Aprili 18 kuwa Coast Starlets ilipata pointi za bwerere baada ya Chaani Ladies kukosa kufika uwanjani Vipingo. Ukweli ni jinsi tulivyochapisha hapa juu.

  • Tags

You can share this post!

PAUKWA: Bahili aokolewa na msamaria mwema

TAHARIRI: Tuharakishe mipango ya kuangamiza viwavijeshi

T L