• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 11:13 AM
Lugogo afurahia kurudi Bandari akitokea Sofapaka

Lugogo afurahia kurudi Bandari akitokea Sofapaka

NA CHARLES ONGADI

KIUNGO wa zamani Bandari FC Wilberforce ‘Zuma’ Lugogo anatarajiwa kurudi kikosini baada ya kuichezea Sofapaka FC kwa msimu mmoja kwa mkopo.

Lugogo aliyejiunga na Sofapaka mwishoni mwa mwaka 2021 alikamilisha mkataba wake wa mkopo katika timu ya Sofapaka Juni 11.

“Nimefurahi msimu ujao nitakuwa katika timu yangu iliyonilea ya Bandari na nitafanya kila juhudi kusaka nafasi katika kikosi cha kwanza,” akasema Lugogo.

Lugogo anakumbukwa alivyotifua vumbi akiwa Bandari mwaka wa 2019 kwa pasi zake nyerezi na kuisaidia timu hiyo kuibuka ya pili katika msimamo wa ligi kuu kutokana na uwezo wake wa kumiliki boli na kutoa pasi za uhakika.

Lugogo ameiambia Taifa Leo kwamba kiu yake kuu kwa sasa ni kuiona Bandari ikinyanyua taji la ligi kuu nchini kwa mara ya kwanza.

“Nimejifunza mengi kipindi nilichokuwa Sofapaka na bila shaka nimeiva kinyama kukabiliana na ushindani mkali katika kikosi cha Bandari,” akasema.

Lugogo ambaye ni mwanafunzi wa zamani wa shule ya upili ya St Anthony, Kitale anatarajiwa kuleta nguvu na ari mpya katika safu ya kati ya Bandari msimu ujao.

  • Tags

You can share this post!

Sakaja aponyoka, Sonko akihema

Ruto avuna wafuasi eneo la Magharibi

T L