• Nairobi
  • Last Updated May 6th, 2024 4:43 PM
Man-City wadengua Chelsea katika raundi ya tatu ya Kombe la FA

Man-City wadengua Chelsea katika raundi ya tatu ya Kombe la FA

Na MASHIRIKA

MANCHESTER City walitinga raundi ya nne ya Kombe la FA baada ya kuponda Chelsea 4-0 katika pambano lililowakutanisha ugani Etihad mnamo Jumapili.

Ushindi wa Man-City uliwakatia tiketi ya kuvaana na kikosi kitakachotamalaki mchuano wa raundi ya tatu kati ya Arsenal na Oxford United uwanjani Kassam mnamo Januari 9, 2023.

Man-City walifungua ukurasa wa mabao kupitia kwa Riyad Mahrez kabla ya fowadi huyo raia wa Algeria kupachika wavuni goli la pili kupitia penalti. Mabao mengine ya Man-City yalijazwa kimiani na Phil Foden na  Julian Alvarez aliyefunga kupitia penalti.

Kichapo hicho kilimweka kocha Graham Potter katika presha ya kutimuliwa baada ya mashabiki kuanza kuimba nyimbo huku wakilitaja jina la Thomas Tuchel, kocha aliyeshindia Chelsea ufalme wa Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) kabla ya kupigwa kalamu na mmiliki mpya wa kikosi hicho, Todd Boehly, mnamo Septemba.

Chelsea sasa wamebanduliwa na Man-City kwenye makombe mawili – Carabao na FA. Masogora hao wa Potter watahitaji sasa miujiza ya kukomoa Borussia Dortmund ili kusalia katika kipute cha UEFA muhula huu.

Chelsea walitua ugani Etihad kwa mechi ya raundi ya tatu ya Kombe la FA wakilenga kulipiza kisasi dhidi ya Man-City waliowapokeza kichapo cha 1-0 katika Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) mnamo Januari 5, 2023.

MATOKEO YA KOMBE LA FA (Jumapili):

Bristol City 1-1 Swansea

Derby 3-0 Barnsley

Cardiff 2-2 Leeds

Hartlepool 0-3 Stoke

Norwich 0-1 Blackburn

Stockport 1-2 Walsall

Aston Villa 1-2 Stevenage

Man-City 4-0 Chelsea

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Barcelona yazamisha Atletico na kufungua pengo la alama...

BENSON MATHEKA: Hatua za Ruto kumaliza ufisadi zisihujumiwe...

T L