• Nairobi
  • Last Updated May 7th, 2024 9:48 PM
Muujiza wa Conte kutoa maji kwenye mwamba pale Spurs

Muujiza wa Conte kutoa maji kwenye mwamba pale Spurs

Na MASHIRIKA

HATA baada ya kuanza kazi kwa ushindi wa 3-2 dhidi ya Vitesse ya Uholanzi katika michuano ya kipute cha Europa Conference League, kocha Antonio Conte wa Tottenhan Hotspur amewataka mashabiki wa klabu hiyo wawe na subira.

“Nahitaji muda nielewane na wachezaji ndipo niweze kufanya kazi nzuri. Kuna mengi ambayo nahitaji kukifanyia kikosi hiki ikiwa ni pamoja na kuleta vifaa vipya vichacahe vitakavyoongezea timu nguvu.

“Vilevile, wachezaji lazima waelewe ninavyotaka ili tufaulu sote,” Conte aliwaambia waandishi wa habari.“Tutahitaji kuwa na utulivu kwa sababu kikosi hiki kinahitaji marekebisho mbalimbali,” aliongeza mkufunzi huyo aliyechukua usukani baada ya Nuno Espirito kutimuliwa Jumatatu iliyopita.

Espirito, ambaye msimu uliopita alikuwa akiwanoa Wolves, alifutwa kazi kutokana na presha ya mashabiki kufuatia matokeo duni.

You can share this post!

Sasa Man-United yakanusha madai kumhusu Ronaldo

Albania kichinjioni Uingereza leo Italia ikitifuana na...

T L