• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 6:07 PM
Real Madrid wadengua vipusa wa Man-City kwenye gozi la UEFA

Real Madrid wadengua vipusa wa Man-City kwenye gozi la UEFA

Na MASHIRIKA

ALIYEKUWA fowadi wa Manchester City, Caroline Weir, alisaidia Real Madrid kudengua waajiri wake hao wa zamani kwenye raundi ya kwanza ya kufuzu kwa kipute cha Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) msimu huu wa 2022-23.

Weir aliyechezea timu ya wanawake ya Man-City mara 66 katika kipindi cha miaka minne, alifungia Real bao la pekee na la ushindi kunako dakika ya 15.

Deyna Castellanos wa Man-City alishuhudia kombora lake likigonga mwamba wa goli la Real huku Esme Morgan akipoteza nafasi kadhaa za wazi za kusawazishia waajiri wake.

Real wanafuzu sasa kwa raundi ya pili ya mchujo wa UEFA msimu huu ambapo watakutana na Arsenal waliokamilisha kampeni za Ligi ya Wanawake nchini Uingereza (WSL) katika nafasi ya pili mnamo 2021-22.

Real wangalifunga mabao zaidi katika kipindi cha pili ila makombora yao yakapanguliwa na kudhibitiwa vilivyo na kipa wa Man-City, Ellie Roebuck.

Man-City walishuka dimbani kuvaana na Real wiki moja baada ya kupepeta Tomiris-Turan ya Kazakhstan 6-0.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Man-City na Newcastle nguvu sawa katika EPL ugani St...

Ghasia za uchaguzi ni jambo geni Lamu

T L