• Nairobi
  • Last Updated May 8th, 2024 4:26 PM
Ronaldo abeba Man-United dhidi ya Norwich City

Ronaldo abeba Man-United dhidi ya Norwich City

Na MASHIRIKA

CRISTIANO Ronaldo alifunga mabao matatu katika ushindi wa 3-2 dhidi ya Norwich City kwenye Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) mnamo Jumamosi ugani Old Trafford na kuweka hai matumaini yao ya kufuzu kwa soka ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) msimu ujao.

Norwich wanaokodolea macho hatari ya kuteremshwa ngazi mwishoni mwa msimu huu, walipata mabao yao kupitia kwa Kieran Dowell na Teemu Pukki.

Ronaldo, 37, anajivunia mabao 15 katika kampeni za EPL msimu huu huku akisoma migongo ya Mohamed Salah na Son Hueng-min wanaochezea Liverpool na Tottenham Hotspur mtawalia. Nyota huyo raia wa Ureno sasa amepachika wavuni mabao 99 kutokana na mechi za EPL.

Man-United watapaa zaidi ligini na kufikia Spurs katika nafasi ya nne kwenye jedwali la EPL iwapo watashinda Liverpool uwanjani Anfield mnamo Aprili 19, 2022.

Norwich almaarufu The Canaries, sasa wanavuta mkia wa jedwali la EPL kwa alama 21 baada ya mechi 32. Imesalia michuano sita pekee kabla ya kampeni za EPL msimu huu kutamatika rasmi.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Dereva Kimathi atarajia Croatia Rally

Liverpool yadengua Man-City FA

T L