• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 6:07 PM
Son Heung-min asaidia Tottenham kuingia raundi ya 16-bora ya Kombe la FA

Son Heung-min asaidia Tottenham kuingia raundi ya 16-bora ya Kombe la FA

Na MASHIRIKA

FOWADI Son Heung-min alipachika wavuni mabao mawili na kusaidia waajiri wake Tottenham Hotspur kuingia raundi ya 16-bora ya Kombe la FA baada ya kukomoa Preston North End 3-0 ugenini.

Spurs, ambao ni mabingwa mara nane wa Kombe la FA, walifunga bao jingine kupitia kwa sajili mpya Arnaut Danjuma aliyetokea Villareal ya Uhispania kwa mkopo wiki hii. Kocha Antonio Conte alikifanyia kikosi chake cha Spurs kilichopepeta Fulham 1-0 katika EPL wiki moja iliyopita mabadiliko saba.

Droo ya hatua ya 16-bora ya Kombe la FA msimu huu itafanyika leo usiku baada ya West Ham United kuvaana na Derby County ugenini.

Son ambaye sasa amefungia Spurs mabao saba katika mashindano yote ya msimu huu, amekuwa akisuasua pakubwa muhula huu. Aliibuka mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) mnamo 2022-23 baada ya kupachika wavuni jumla ya mabao 23.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Shujaa kuvaana na Fiji, Australia na Japan raga ya Los...

Casemiro abeba Manchester United dhidi ya Reading katika...

T L