• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 6:07 PM
VITUKO: Neuer ajiandaa kuishi na Anika raha mustarehe

VITUKO: Neuer ajiandaa kuishi na Anika raha mustarehe

IMETAYARISHWA NA CHRIS ADUNGO

GOLIKIPA na nahodha wa Bayern Munich na timu ya taifa ya Ujerumani, Manuel Neuer, sasa anajiandaa kuishi raha mustarehe na mpenzi wake Anika Bissel, 21.

Neuer, 36, alianza kudokoa tunda la Anika mwanzoni mwa 2020, miezi minne pekee baada ya kubwagana rasmi na mkewe Nina Weiss anayelandana na Anika kama shilingi kwa ya pili.

Neuer alitumia mtandao wake wa Instagram kupakia baadhi ya picha alizopigwa pamoja na Anika na kuandika: “Natazamia siku nitakapokufanya wangu wa halali, tule yamini ya ndoa na tuanze kufyatua watoto. Nitaona raha mamangu Marita akipata wajukuu zaidi.”

Anika ni mtaalamu wa masuala ya ulimbwende na fasheni jijini Munich na mchezaji wa handiboli katika klabu ya Kuties, Ujerumani.

Neuer aliwahi pia kuchovya asali kwenye mzinga wa kidosho Kathrin Glich hadi mwaka wa 2014.

Alianza kumchumbia Nina mnamo 2015 na wakafunga pingu za maisha mnamo Mei 21, 2017.

  • Tags

You can share this post!

Okutoyi tayari kutafuta ufanisi katika mechi ya mchezaji...

Arsenal watandika Bournemouth na kuendeleza ubabe wao...

T L