• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 9:35 PM
Voliboli: KPA, Kenya Army zatolewa kijasho

Voliboli: KPA, Kenya Army zatolewa kijasho

Na JOHN KIMWERE

TIMU ya wanaume ya Halmashauri ya Bandari ya Kenya (KPA) iliandikisha ushindi wa pili kwenye mechi za mkondo wa pili za Ligi Kuu ya Voliboli zilizopigiwa ugani Nyayo Stadium, Nairobi.

Nayo Kenya Army ya kocha, William Wahome ilitoka chini kwa kufungwa seti moja na kuvuna ufanisi wa seti 3-2 mbele ya Administration Police(AP Kenya) kwenye mechi yakusisimua. Madume wa KPA walizaba Prisons Nyanza seti 3-1.

Kikosi hicho chini ya nahodha, Sammy Ngeny kilipoteza seti ya kwanza kwa alama 22-25 kabla ya kufufua mchezo wacho na kushinda kwa alama 25-16, 25-18, 25-20. KPA ilikuwa bila huduma za Enock Mogeni anayeshiriki dhoruba ya kulipwa nchini Misri akichezea klabu ya Smouha. Hata staa wao Elijah Bosire alifanya kazi ya kupendeza na kusaidia kubeba ushindi huo.

”Ninashukuru vijana wangu kwa ushindi huo lakini hawakucheza jinsi nilivyotarajia,” kocha wa KPA, Sammy Mulinge alisema na kuongeza kuwa leo (Jumapili) wanatarajia mechi ngumu watakapokutanishwa na Kenya Army. Kenya Army ilipata alama za 17-25, 25-23, 21-25, 25-21, 15-11.

”Hakuna kulegeza kamba tunataka ushindi kwenye mechi zetu zote ambapo tumepangwa kucheza na KPA leo (Jumapili),” kocha wa Army alisema. Kwenye matokeo mengine, Nairobi Prisons ilipiga Prisons Western seti 3-0 (25-21, 25-17, 26-24). Nao washiriki wapya Trailblazers walivuna seti 3-2 (23-25, 25-18, 15-25, 26-24, 16-14) dhidi ya Equity Bank.

You can share this post!

Uhaba wa ngano wanukia wakulima wakisusia kilimo

Chama cha Jubilee chaanza kampeni kali ya kuvumisha Azimio...

T L