• Nairobi
  • Last Updated May 8th, 2024 5:50 AM
IEBC yasema iko tayari kutii mabadiliko yoyote ya kikatiba endapo yatatokea

IEBC yasema iko tayari kutii mabadiliko yoyote ya kikatiba endapo yatatokea

Na WINNIE ONYANDO

MWENYEKITI wa Tume ya Uchaguzi na Mipaka nchini, IEBC, Bw Wafula Chebukati ametangaza kuwa uchaguzi wa Agosti 2022 utafanyika jinsi ulivyopangwa.

Akitoa makadirio ya bajeti ya uchaguzi mkuu huo, Bw Chebukati alisema kuwa uchaguzi hautaahirishwa bali utafanyika kulingana na Katiba ya Kenya.

“Nimeona mipango ya kujaribu kuahirisha uchaguzi ulivyopangwa. IEBC haitachukua maoni yoyote kutoka kwa mtu yeyote au mashirika kwa kuwa ni tume inayojisimamia,” akasema Bw Chebukati.

Alisema kuwa tume hiyo inaoongozwa na Katiba ya Kenya inayosema kuwa uchaguzi utafanyika Agosti 9, 2022.

Hata hivyo, alisema kuwa ikiwa kutakuwa na mabadiliko yoyote ya kikatiba, basi IEBC itatii.

Uchaguzi huo unatarajiwa kuchukua Sh40.19 bilioni.

You can share this post!

UDAKU: Huyu Neymar hapoi, amedakia Bruna kabla Natalia...

MBWEMBWE: Kigogo Chiellini ana noti za kukausha bahari nzima