NA MAUREEN ONGALA
MBUNGE wa Malindi, Bi Aisha Jumwa, amewakejeli waliokuwa wakidai hataidhinishwa kuwania ugavana Kilifi kwa sababu ya kesi zinazomwandama.
Akizungumza Jumapili baada ya kupokezwa cheti cha uwaniaji na IEBC, Bi Jumwa anayewania kupitia kwa UDA alisema ana mipango bora ya kimaendeleo.
IEBC ilimwidhinisha pia Bw Gideon Mung’aro anayewania ugavana kwa tikiti ya ODM.