Na VALENTINE OBARA
SENETA wa zamani wa Mombasa, Bw Omar Hassan, amependekeza kuwa Mbunge wa Malindi, Bi Aisha Jumwa, awe naibu kiongozi wa Chama cha United Democratic Alliance (UDA) wakati viongozi watachaguliwa rasmi.
Kulingana naye, mbunge huyo amesimama kidete kutetea haki za Wapwani. Alimtaka Naibu Rais William Ruto aunge mkono pendekezo hilo.
ili kudhihirisha Pwani ina nafasi bora katika UDA na vile vile kuleta usawa wa kijinsia katika uongozi wa chama.