• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 1:22 PM
Mvurya ampigia naibu wake debe

Mvurya ampigia naibu wake debe

NA WINNIE ATIENO

GAVANA wa Kwale Salim Mvurya amewasihi wakazi kumpigia kura naibu wake Bi Fatuma Achani akisema atamaliza miradi yote ya maendeleo ambayo hayajakamilika.

Bw Mvurya alitoa mfano wa barabara ya Samburu-Chengoni ambayo alisema itakamilishwa baada ya uchaguzi mkuuwa Agosti wakati Bi Achani atakuwa amechaguliwa.

“Bi Achani ataendeleza ruwaza yangu, amekuwa naibu wangu tangu 2013, amekuwa mwaminifu na mkimpigia kura ataendeleza kazi yangu nzuri.ā€¯ikiwemo barabara, hospitali, shule na maendeleo mengine,” alisema.

Bi Achani naye aliwasihi wakazi kumuunga mkono akiapa kutimiza ahadi ya maendeleo.

“Nawaomba munipigiei kura niendeleze kazi yetu nzuri. Pigeni kura mahali maslahi yenu yatashughulikiwa. Msipige kura sababu ya kushawishiwa na pesa au mwaniaji ni kabila lako au jinsia yako,” alisema.

Alikana madai kuwa amewasimamisha kazi wafanyikazi wa jamii ya waduruma.Bi Achani alisema hana mamlaka ya kuajiri wala kumsimamisha mtu kazi.

“Hilo ni jukumu la gavana kwa hivyo wacheni urongo kuwa nimefuta watu kazi kutoka jamii yoyote,” alisema alipoandamana na mgombea mwenza Chirema Kombo wakiomba kura.

  • Tags

You can share this post!

Vyuo vikuu vya umma kuzidi kuumia kifedha

Msisimko Mlima Kenya Spika Muturi akizungumza lugha ya...

T L