• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 2:00 PM
Ruto amponda Raila kuhusu mitumba

Ruto amponda Raila kuhusu mitumba

NA MANASE OTSIALO

NAIBU Rais William Ruto amemsuta mgombea urais wa Muungano wa Azimio la Umoja One Kenya Raila Odinga kuhusu uagiziaji wa nguo za mitumba nchini.

Akiwa kwenye msafara wa kampeni mjini Mandera, mgombea urais huyo wa United Democratic Alliance (UDA) alimsuta Bw Odinga kwa kusema kwamba ikiwa atachaguliwa, atapiga marufuku uagizaji wa mitumba na badala yake kuimarisha viwanda vya kutengeza mavazi nchini.

“Mshindani wetu alisema juzi kuwa wale wanaouza mitumba wanajishughulisha na bidhaa za waliokufa. Hiyo ni kukosa uhalisia kwa wananchi wetu na ninataka kuwaeleza wafanyabiashara wa mitumba kwamba serikali yangu itaunga mkono kazi yenu,” alisema.

Dkt Ruto alisema ikiwa atachaguliwa, wauzaji wote wa mitumba watasajiliwa katika vyuo vya ufundi ili kuunda nguo nchini.

“Kupitia mpango wa kukuza uchumi tutawezesha wafanyabiashara wote wa mitumba kuwa wawekezaji katika sekta ya mavazi nchini,” akasema.

Alipokuwa akizindua manifesto yake katika mnamo Jumatatu usiku, kiongozi wa ODM alisema mavazi ya mitumba yanayovaliwa na Wakenya yalikuwa yakivaliwa na watu waliokufa.

  • Tags

You can share this post!

Maoni yaweka Raila hatua kadhaa mbele ya Ruto

Sonko azidi kusukuma IEBC muda ukiyoyoma

T L