• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 9:35 PM
Ruto kuzuru tena ngome ya Raila kwa hafla ya Owalo kukaribishwa nyumbani

Ruto kuzuru tena ngome ya Raila kwa hafla ya Owalo kukaribishwa nyumbani

NA JUSTUS OCHIENG

RAIS William Ruto anatarajiwa kuongoza ujumbe wa serikali katika Kaunti ya Siaya, ambayo ni ngome ya kisiasa ya kinara wa Azimio la Umoja, Raila Odinga, Jumamosi ijayo, kwa hafla ya makaribisho ya Waziri wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT), Eliud Owalo.

Duru katika Ikulu zilisema jana kuwa tayari viongozi kutoka eneo hilo wamefahamishwa kuwa Rais atafanya ziara katika eneo hilo.

Hapo jana Jumapili, Bw Owalo hakutaka kutoa maelezo kuhusu ziara hiyo, ijapokuwa alithibitisha kuwa atawaalika Wakenya kuhudhuria hafla hiyo Jumamosi, nyumbani kwake katika eneo la Asembo, eneobunge la Rarieda.

“Jumamosi, Januari 14 imethibitishwa kuwa siku ya makaribisho yangu eneo la Asembo, eneobunge la Rarieda, Kaunti ya Siaya. Mnakaribishwa kwa hafla hiyo itakayoanza saa tatu asubuhi,” akasema Bw Owalo.

Alisema hafla hiyo itafanyika nyumbani kwa marehemu baba yake, Askofu Gideon Charles Owalo wa Kanisa la Nomiya, Asembo, Rarieda, ambapo itawaleta pamoja viongozi kutoka mirengo yote ya kisiasa.

“Hafla hiyo itafanyika Jumamosi ambapo viongozi na Wakenya kutoka tabaka zote wamekaribishwa,” akasema.

Ziara hiyo ndiyo itakuwa ya pili kwa Rais Ruto katika eneo hilo baada ya nyingine aliyofanya Oktoba katika Kaunti ya Homa Bay mwaka 2022.

  • Tags

You can share this post!

Raila ataka Ruto amtafute ikiwa anataka kubadili Katiba

Wanafunzi 600 kutoka Landi Mawe wanufaika na basari kutoka...

T L