NA GEORGE ODIWUOR
ALIYEKUWA gavana wa Nairobi Dkt Evans Kidero (pichani), amelalamika kuwa wapinzani wake wanatishia wapigakura kwa kuwaambia kwamba hatatangazwa mshindi wa uchaguzi mkuu wa Agosti 9, hata akipata kura nyingi kuliko wagombeaji wengine.
Alidai baadhi ya wanasiasa wanaeneza habari za uongo kwamba mshindi wa uchaguzi mkuu ujao tayari anajulikana na kwamba watu fulani watatangazwa washindi katika kaunti ya Homa Bay.
Dkt Kidero ambaye anagombea ugavana kaunti hiyo kama mwaniaji huru anashindana na Mwakilishi wa Wanawake kaunti ya Homa Bay Gladys Wanga wa chama cha ODM. Amewataka wakazi kupuuza habari hizo na wajitokeze kupiga kura kwa wingi.