NA JANET KAVUNGA
BOMBOLULU, MOMBASA
KALAMENI wa hapa anawazia kutafuta mpango wa kando kwa sababu ya kile anachotaja kama hatua ya mkewe ya kususia shughuli za ndoa baada ya kupandishwa cheo kazini.
Kulingana na jamaa, kabla ya kupandishwa cheo kuwa bosi katika kampuni anayofanya kazi, mkewe alikuwa akichangamkia shughuli chumbani lakini alibadilika ghafla baada ya kupata wadhifa mkubwa.
“Hanithamini chumbani. Hashughuliki nami kamwe na ananidhararu siku hizi kwa kuniona kabwela kwa kuwa sina cheo kama chake. Nitakachofanya ni kutafuta mpango wa kando mrembo sana na niweke wazi uhusiano wetu ili mke wangu aingiwe na wivu,” jamaa aliambia marafiki zake.
Lakini marafiki walimshauri azungumze na mkewe watatue shida iliyopo badala ya kujitosa kwenye michepuko.