NA CORNELIUS MUTISYA
MACHAKOS MJINI
KISANGA kilishuhudiwa mjini hapa, pasta mmoja alipoweka Biblia chini na kumtwanga jamaa aliyetorosha mkewe.
Jamaa huyo alikuwa akifanya kazi nyumbani kwa mhubiri huyo na akaanzisha uhusiano wa kimahaba na mkewe.
Inadaiwa mapenzi yao yalinoga mno na wakatoroka wakaenda kuishi pamoja katika chumba cha kupanga mjini hapa.
Juzi, pasta alikutana na jamaa huyo mjini hapa na wakaanza kupigana akimtaka amweleze alikokuwa mkewe.
Ilibidi wananchi waingilie kati na wakawatenganisha kabla ya kuchafuana sura zaidi.
“Pasta fahamu kuwa maji yakimwagika hayazoleki. Itakubidi uzoee,” mama mmoja alimtania pasta.