• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 12:09 PM
Pasta aweka Biblia kando na kumlima polo aliyemtorosha mkewe

Pasta aweka Biblia kando na kumlima polo aliyemtorosha mkewe

NA CORNELIUS MUTISYA

MACHAKOS MJINI

KISANGA kilishuhudiwa mjini hapa, pasta mmoja alipoweka Biblia chini na kumtwanga jamaa aliyetorosha mkewe.

Jamaa huyo alikuwa akifanya kazi nyumbani kwa mhubiri huyo na akaanzisha uhusiano wa kimahaba na mkewe.

Inadaiwa mapenzi yao yalinoga mno na wakatoroka wakaenda kuishi pamoja katika chumba cha kupanga mjini hapa.

Juzi, pasta alikutana na jamaa huyo mjini hapa na wakaanza kupigana akimtaka amweleze alikokuwa mkewe.

Ilibidi wananchi waingilie kati na wakawatenganisha kabla ya kuchafuana sura zaidi.

“Pasta fahamu kuwa maji yakimwagika hayazoleki. Itakubidi uzoee,” mama mmoja alimtania pasta.

  • Tags

You can share this post!

Infantino anguruma kwa Kiswahili akizindua Ligi ya Kandanda...

Ruto aondoa hitaji la visa kwa raia wa Angola

T L