NA JOHN MUSYOKI
EMBU MJINI
WAPANGAJI wa ploti moja mjini hapa, walipigwa na butwaa machangudoa watatu walipojitoma chumbani kwa landilodi wao na kumlazimisha alipe mmoja wao deni lake.
Akina dada hao walikuwa wakipayuka na mmoja wao akapasua mbarika.
Ilibainika kuwa landilodi huyo alihudumiwa na mmoja wao na kuhepa bila kulipa.
“Unajua dawa ya deni ni kulipa? Uliramba asali na ukapotea ukidhani sitakupata?” kidosho alifoka.
Mke wa landilodi aliposikia mumewe alikuwa mchepukaji alimchemkia pia.
“Sijui wanawake hawa ni akina nani. Ni walevi na pengine wamekosea wanayemtafuta,” jamaa alimrai mkewe.
Akina dada hao walizidi kushinikiza jamaa huku wakitisha kumwaga mtama zaidi hadi akatumia demu pesa kwa simu na kumwambia kupitia arafa ajifanye sio yeye alikuwa akiandama.
Demu alicheza kama yeye asipoteze mteja na wakaondoka.