• Nairobi
  • Last Updated May 16th, 2024 5:50 AM
Demu amenizungusha miezi miwili, anataka zawadi ndipo anipe asali!

Demu amenizungusha miezi miwili, anataka zawadi ndipo anipe asali!

Za kwako shangazi?

Mpenzi wangu amenizungusha kwa miezi miwili akidai zawadi ndipo nionje asali. Kufikia sasa, nimempa zawadi kadhaa na pesa lakini anataka zaidi. Ananipenda kweli?

Ninashuku iwapo kuna mmoja wenu anayempenda mwenzake. Wewe unafikiria tu kuhusu asali huku naye akitafuta zawadi na pesa. Mapenzi ya dhati hayana masharti. Tafakari hayo.

Jamaa anataka kunioa lakini ategemea wazazi

Mpenzi wangu anataka kunioa. Nampenda lakini kuna jambo linanitia wasiwasi. Alimaliza chuo kikuu miaka miwili iliyopita na hashughuliki kutafuta kazi, anategemea wazazi wake. Nishauri.

Una sababu ya kuwa na wasiwasi. Mahitaji ya familia ni mengi na hayawezi kutegemea msaada kutoka kwa wazazi. Shauriana na mpenzi wako ili atafute kazi kwanza.

Mpenzi wangu hanipigii simu wala kunitembelea

Nina mpenzi lakini hatujaonana kwa miezi miwili sasa. Sielewi kwa sababu amekuwa akinitembelea kila wikendi. Hata simu hapigi na nikimpigia huniambia bado ananipenda. Ananicheza?

Dalili ya mvua ni mawingu. Hizo ni dalili za mtu anayeteka kuvunja uhusiano. Hata kama amekosa nafasi ya kukutembelea, anafaa kukupigia simu. Mtafute akwambie kinachoendelea.

Mume wa wenyewe ameniganda licha ya mkewe kugundua

Nimekuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamume aliye na familia. Mke wake amegundua na nimeamua kumuacha. Lakini anasisitiza tuendelee. Waonaje?

Unajua kuwa uhusiano wenu ni haramu na ndio sababu umeingiwa na hofu baada ya kugunduliwa. Kuendelea nao ni kuhatarisha maisha yako kwa sababu hujui mpango wa mkewe. Shauri yako.

  • Tags

You can share this post!

ODM kutuza watakaozuia wakazi kujiunga na UDA Nyanza

Serikali sasa yaweka ada ya kupata kitambulisho kuwa Sh300...

T L