• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 10:50 AM
Nashindwa kuambia mke wangu dadake ni mkora, huenda akasirike

Nashindwa kuambia mke wangu dadake ni mkora, huenda akasirike

SHANGAZI;

Tunaishi mjini na dada ya mke wangu akitafuta kazi. Nimeambiwa amekuwa akileta wanaume nyumbani kwetu. Nahofia nikimwambia mke wangu atafikiria namchukia dada yake. Nishauri.

Hata kama hutaki kumkwaza mke wako, kuna mambo unafaa kuzingatia. Watoto wenu wanaweza kuathiriwa na tabia hiyo iwapo ni kweli. Ni heri umwambie ili achunguze na akithibitisha achukue hatua inayofaa.

Nina mimba yake lakini sitaki kuwa mkewe

Nina mimba ya mpenzi wangu. Nimeamua hawezi kuwa mume wangu kwa sababu sina hakika kuhusu mapenzi yangu kwake. Sasa nahofia atatumia mtoto kunilazimisha katika ndoa. Nishauri.

Sielewi kauli yako eti humpendi mwanamume huyo ilhali umekubali kupata mimba yake. Hata hivyo, hawezi kukulazimisha kuwa mke wake. Mwambie hivyo ili muachane. Suala la mtoto mtasuluhisha nje ya ndoa.

Wanaume wanipigania ilhali sijakubali yeyote

Nina marafiki wengi wa kiume na baadhi yao wamekuwa wakitaka tuwe wapenzi. Kumezuka uadui kati yao
kuhusu penzi langu ingawa sijamkubali yeyote. Nifanyeje?

Iwapo hujaamua kuwa na mpenzi, ni muhimu umwambie kila mmoja wao ili kukomesha uhasama huo. Na kama umeamua, ni muhimu pia utangaze msimamo wako kuhusu unayempenda ili wengine wajiondoe.

Nilimwacha mpenzi kwa dai alikuwa na mwingine, nimegundua ulikuwa uwongo, ninajuta

Nilimwacha mpenzi wangu niliposikia alikuwa na mwingine. Lakini baadaye niligundua ulikuwa uzushi. Bado nampenda na yuko tayari kunioa. Ingawa nimeolewa na mume wangu hajanikosea nimechanganyikiwa, nishauri.

Ulikosea kuacha chaguo la moyo wako kwa sababu ya udaku. Sasa wewe ni mke wa mtu lakini moyo wako uko kwa mwingine. Itabidi uchague kutulia katika ndoa yako ama utoke uolewe na huyo wa zamani.

  • Tags

You can share this post!

Kipusa Ntalami ashtaki kipindi cha televisheni kutumia...

Kinaya Nairobi ikipanga kununua maboti kudhibiti athari za...

T L