• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 3:55 PM
Tanzania yailemea Kenya katika uvutaji bangi – Utafiti

Tanzania yailemea Kenya katika uvutaji bangi – Utafiti

Na MWANGI MUIRURI 

Kenya imeorodheshwa katika nafasi ya sita kuhusu ubingwa wa uvutaji bangi.

Mwanasiasa George Wajackoyah huipigia debe ihalalishwe akisema ni mmea wa faida na ambao unaweza ukasaidia taifa hili kulipia madeni yake katika kipindi kifupi cha baada ya uzinduzi wa kuikuza.

Hata hivyo, msimamo huo wa Wajackoyah haujaungwa mkono na utafiti wowote wa kuaminika huku Wakenya wengi wakimkataa katika azima yake ya kuwa Rais katika uchaguzi mkuu wa Agosti 9, 2022 ambapo alipata chini ya asilimia moja ya kura.

Kulingana na utafiti wa kitengo cha Afya na Elimu cha Marekani, waliolemea Kenya katika uvutaji wa bangi ni raia wa Nigeria ambapo miongoni mwa raia wkee, watu milioni 20.8  huivuta.

Ethiopia ndio wa pili ambapo raia milioni 7.1 huivuta huku Misri ikiwa na watu milioni 5.9 ambao ni waraibu wa mihadarati hiyo.

Taifa la DR Congo limeorodheshwa la nne Afrika likiwa na wavutaju milioni 5, Tanzania likiwa na wavutaji milioni 3.6 huku Kenya ikiridhika na nafasi ya sita kwa kuwa na waraibu milioni 3.3.

Taifa la Sudan liko katika nafasi ya saba kwa kuwa na wapenda bangi  milioni 2.7 huku taifa la Uganda likiwa na wavutaji milioni 2.6.

Madagascar wako na wapenda bangi milioni 2.1 nao Ghana wakifunga orodha ya kumi bora kwa kuwa na wanabangi milioni 2.

Duniani, Marekani, Canada, Nigeria na Australia raia katika mataifa hayo walirekodiwa kupenda bangi sana hasa katika wale walio na miaka 15 kwenda juu.

Ripoti ya Umoja wa Mataifa ya 2021 ilikuwa imeonya kwamba wavutaji bangi Afrika walikuwa wakiongezeka kwa kasi na huenda watinge asilimia 40 kabla ya 2030.

Zimbabwe, Malawi, Niger na Zambia ni mataifa ambayo yamesemwa kuwa na wapenda bangi wachache wakiwa ni milioni 1.1, 1.2, 1.2 na 1.4 mtawalia.

Hata hivyo, ripoti hizo zote zinaonya kwamba uraibu wa bangi ni hatari kwa afya ya watumizi, kusambaratikiwa na akili kukiwa ndio athari kuu.

[email protected]

  • Tags

You can share this post!

Eric Omondi aomboleza kupoteza mtoto aliyetaka kusaidia...

Naibu Spika ataka polisi sasa waanze kuvalia kamera mwilini...

T L