• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 6:07 PM
Viongozi waahidi kampeni za amani Rift Valley

Viongozi waahidi kampeni za amani Rift Valley

Na KNA

VIONGOZI wa kisiasa Rift Valley wameapa kuendesha kampeni za amani kabla, wakati na baada ya uchaguzi mkuu ujao.

Wakizungumza katika shule ya msingi ya Siwot, Bomet wakati wa ibada kabla ya mazishi ya mamake katibu mkuu wa Kanu, Nick Salat, viongozi hao walisema amani ni muhimu kwa eneo lao na nchi kwa jumla.

Gavana wa Nakuru Lee Kinyanjui alisema kwamba mashirika ya usalama yamekuwa yakiorodhesha Rift Valley kama kitovu cha ghasia za uchaguzi lakini hali itakuwa tofauti mwaja ujao.

Alisema licha ya kuwa na mirengo tofauti ya kisiasa, kuna haja ya kuruhusu watu kuchagua viongozi wanaowataka.

Mbunge wa kuteuliwa Wilson Sossion alisema kwamba wakati umefika wanasiasa washiriki kampeni za amani kwa kuangazia masuala tofauti badala ya kuchochea ghasia.

Kiongozi wa Chama cha Mashinani (CCM) Isaac Rutto alisema kwamba uchaguzi ujao unafaa kuwa wa amani.

  • Tags

You can share this post!

Kibicho atajwa katika masaibu ya Ngirici UDA

Raila aahidi kutunza misitu ya Kaya akishinda urais,...

T L