• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 6:07 PM
Ababu ataka wabaya wa Azziad wakome kuzua madai ya uongo dhidi yake

Ababu ataka wabaya wa Azziad wakome kuzua madai ya uongo dhidi yake

NA RICHARD MAOSI

WAZIRI wa Michezo Ababu Namwamba amevunja ukimya na kuweka wazi kwamba kivyovyote vile, hayuko kwenye uhusiano wa kimapenzi na staa wa TikTok Azziad Nasenya.

Amewakemea wambea, akisema haelewi ni kwa nini baadhi ya Wakenya wamekuwa wakisambaza propaganda.

Anasema si haki kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii kuendelea kumrushia Azziad mikuki.

“Namsikitikia sana binti mdogo. Yeye huenda hana uvumilivu kama mimi. Binafsi nimeishi kuona mengi katika ulimwengu huu ambao umegeuzwa ukawa ni tambara bovu na nikakomaa na safari,” akasema huku akisisitiza kwamba hana muda na vijimambo.

Alieleza ingawa ni jukumu la wananchi kufuatilia kwa makini utendakazi wa viongozi na hata mitindo ya maisha ya wasanii na mastaa wengine, si vyema kusambaza madai ya uongo.

“Mbona mtu amharibie mwenzake jina?” akauliza waziri Namwamba.

Azziad alipata umaarufu baada ya kutumia weledi na ubunifu wake mtandaoni kuvutia mashabiki.

Lakini wakati mwingine anajipata pabaya kwa sababu mara si moja ‘wabaya wake’ hawaishi kumpiga vijembe mtandaoni.

Amewahi kukiri kuwa nusura atumbukie kwenye msongo wa mawazo.

Pia amelazimika kuchukua hatua za kisheria kukabiliana na baadhi ya watu, ambao alihisi wamemkosea na kumchafulia jina.

  • Tags

You can share this post!

Mwanamume afariki siku moja kabla ya kufunga pingu za maisha

Duale afika Lamu kuziba vichochoro vya Al-Shabaab

T L