NA MWORIA MUCHINA
BUIBUI wanaofahamika kama Bird-eating spiders ambao jina la kisayansi ni Theraphosa blondi huwa wakubwa sana kimaumbile.
Wana nywele kama mishale kwenye ngozi zao na hizi nywele huwa na sumu kali.
Hawa ndio buibui wakubwa duniani na wana meno marefu sana miongoni mwa buibui.
Hula viumbe kama wadudu, ndege wadogo na viumbe wengine. Wanaweza wakakaa wiki moja bila kula. Kujikinga dhidi ya maadui, buibui hawa wanaweza kurusha nywele hizo zinazofanana na mishale ambazo huwa na sumu kali.