• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 6:07 PM
Salasya: Natafuta mwanamke Mzungu wa kuoa

Salasya: Natafuta mwanamke Mzungu wa kuoa

NA MERCY KOSKEI

Mbunge wa Mumias Mashariki Peter Salasya amefichua kuwa anatafuta mwanamke Mzungu wa kuchumbiana naye.

Mwanasiasa huyo mcheshi kupitia kwa mtandao wake wa kijamii wa Twitter Alhamisi Septemba 28, 2023, alichapisha kuwa anataka kuoa mwanamke mzungu, jambo lililoibua hisia tofauti mitandaoni.

“Nimetamani sana kuchumbiana na mwanamke mzungu kwa muda mrefu. Nataka mwanamke Mzungu kutoka nchi yoyote. Bora tu awe mzungu. Awe mwembamba kati ya miaka 20-26. Zaidi ya miaka 30 atakuwa amesonga sana. Hao wanasumbua. (Sitaki mtu zaidi ya 30. Wana ukaidi sana),” aliandika.

Mbunge huyo wa mara ya kwanza mwenye umri wa miaka 33, hata hivyo, hakutaja kiwango cha masomo ambayo mwanamke huyo anafaa kuwa nayo, ila alisema kuwa anafaa kuwa tayari tu kuhamia Kenya.

Mnamo Septemba 2022, baada ya kuchaguliwa, katika mahojiano na mojawapo ya vyombo vya habari, mbunge huyo alifichua kuwa mitandao yake ya kijamii, ulikuwa umejaa ujumbe na picha chafu kutoka kwa wanawake waliokua wanamwandama.

Salasya alifichua kwamba mpenzi wake wa zamani alimtema na kuendea tajiri mmoja mwaka wa 2017 baada ya kushindwa kunyakua kiti cha ubunge.

“Tulikuwa tumechumbiana kwa miezi saba, lakini baada ya kushindwa katika Uchaguzi Mkuu wa 2017, aliniacha kwa sababu sikuwa na pesa za kumkimu, bado yuko kwenye ndoa,” alifafanua.

Mnamo Machi, Salasya alifichua kuwa bado hajapata nafasi ya kuchumbiana au hata kuoa kwa sababu ya majukumu kadhaa ya kiserikali.

Alieleza kuwa bado hajaoa kwa sababu hana muda wa kuwatongoza wanawake.

  • Tags

You can share this post!

Maeneo bunge yasiyo na idadi tosha ya watu kumezwa

Kero kwa Zuchu Tanasha Donna akimpa Mama Dangote zawadi ya...

T L