Atalanta yapiga AC Milan breki kali ligini
REKODI iliyoshuhudia AC Milan wakishinda mechi saba mfululizo katika kampeni za Ligi Kuu ya Italia (Serie A) ilipigwa breki na Atalanta waliowalazimishia sare ya 1-1 mnamo Jumapili.
Ruslan Malinovskyi aliwaweka Atalanta kifua mbele katika dakika ya 29 kabla ya Ismael Bennacer aliyeshirikiana na Alexis Saelemaekers kusawazishia Milan kunako dakika ya 68.
Napoli na Inter Milan wanaselelea kileleni mwa jedwali la Serie A kwa alama sita kila mmoja baada ya kushinda mechi mbili za ufunguzi wa muhula huu wa 2022-23.
Milan ambao ni mabingwa watetezi wa Serie A, wanajivunia alama nne ikizingatiwa kwamba walifungua msimu kwa ushindi wa 4-2 dhidi ya Udinese. Masogora hao wa kocha Stefano Pioli, walinyanyua taji la Serie A kwa mara ya kwanza baada ya miaka 10 mnamo 2021-22 baada ya kuwapiga kumbo Inter kwa alama mbili pekee.
Mara ya mwisho kwa Milan kushinda taji la Serie A mara mbili mfululizo ni 1992-93 na 1993-94.
MATOKEO YA SERIE A (Jumapili):
Bologna 1-1 Hellas Verona
Next article
ZARAA: Ukuzaji wa matunda wazima ‘ushawishi’ wa zao la...