• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 7:50 AM
Bruno Fernandes aponea kwenye ajali ya gari barabarani

Bruno Fernandes aponea kwenye ajali ya gari barabarani

Na MASHIRIKA

KIUNGO Bruno Fernandes wa Manchester United hakuumia baada ya gari lake kuhusika kwenye ajali ya barabarani akielekea mazoezini.

Hakuna yeyote kati ya waliokuwa katika gari lililogongana na lake alipata majeraha mabaya. Baada ya tukio hilo la Aprili 18, 2021, Fernandes, 27, alifululiza hadi uwanjani na akashiriki vipindi vya mazoezi na wanasoka wenzake kambini mwa Man-United kama kawaida.

“Fernandes yuko sawa na atakuwa sehemu ya kikosi tutakachokitegemea dhidi ya Liverpool ugani Anfield mnamo Aprili 19, 2021,” akasema kocha mshikilizi wa Man-United, Ralf Rangnick.

Liverpool ya kocha Jurgne Klopp kwa sasa kinashikilia nafasi ya pili kwenye msimamo wa jedwali la Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) kwa alama 73, moja nyuma ya viongozi na mabingwa watetezi, Manchester City. Man-United kwa upande wao wanakamata nafasi ya tano huku pengo la pointi tatu likitamalaki kati yao na nambari nne Tottenham Hotspur.

Fernandes amefungia Man-United mabao tisa na kuchangia sita mengine kutokana na mechi 30 ambazo amechezea Man-United msimu huu.

Ushirikiano mkubwa kati ya Cristiano Ronaldo na Fernandes ambaye pia ni raia wa Ureno ulichangia ushindi wa 3-2 uliosajiliwa na waajiri wake dhidi ya Norwich City katika mchuano uliopita wa EPL ugani Old Trafford.

Msemaji wa Halmashauri ya Huduma za Wazimamoto katika eneo la Great Manchester alisema: “Tuliarifiwa kuhusu ajali iliyohusisha magari mawili katika eneo la School Lane, Dunham Massey na kikosi chetu kikafika huko haraka. Magari yaliharibika na ilihitaji takriban dakika 45 kuyaondoa barabarani.”

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

MAKALA MAALUM: Wazee wa Kaya watakasa eneo la ujenzi wa...

Wakili bandia taabani kwa kumwakilisha mganga kutoka Ghana

T L