• Nairobi
  • Last Updated May 7th, 2024 9:48 PM
Mbappe afunga mawili na kusaidia PSG kurefusha mkia wa Dijon katika jedwali la Ligue 1

Mbappe afunga mawili na kusaidia PSG kurefusha mkia wa Dijon katika jedwali la Ligue 1

Na MASHIRIKA

KYLIAN Mbappe alifunga mabao mawili na kusaidia waajiri wake Paris Saint-Germain (PSG) kuwacharaza Dijon wanaovuta mkia wa Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) 4-0 mnamo Februari 27, 2021.

Moise Kean anayechezea PSG kwa mkopo kutoka Everton aliwafungua karamu hiyo ya mabao katika dakika ya sita kabla ya Mbappe kuongeza la pili kunako dakika ya 32 kupitia mkwaju wa penalti.

Fowadi huyo chipukizi raia wa Ufaransa alipachika wavuni goli la tatu la PSG katika dakika ya 51 kabla ya Danillo kuzamisha kabisa chombo cha wenyeji wao mwishoni mwa kipindi cha pili.

Mbappe kwa sasa anajivunia rekodi ya kufungia PSG jumla ya mabao 113. Mshambuliaji Julian Draxler alipoteza nafasi nyingi za wazi ambazo zingevunia PSG mabao zaidi katika kipindi cha pili.

Chini ya kocha Mauricio Pochettino, PSG kwa sasa wanashikilia nafasi ya pili jedwalini kwa alama 57, moja nyuma ya viongozi Lille watakaochuana na Strasbourg katika mojawapo ya mechi za Ligue 1 mnamo Februari 28.

MATOKEO YA LIGUE 1 (Februari 27):

Dijon 0-4 PSG

Bordeaux 1-2 Metz

You can share this post!

Messi aongoza Barcelona kupepeta Sevilla ligini na...

Sancho aweka rekodi ya uchangiaji mabao katika soka ya...